Fadhili na upendo ni miongoni mwa hisia za kwanza ambazo mtu hupokea na kuelewa akiwa mtoto mchanga na kukua nazo.
Kuna aina mbili za wema:
Nabii Nuh au Nuhu (AS), ambaye alikuwa miongoni mwa mitume wakubwa wa Mwenyezi Mungu, alitumia njia ya wema na hurumakuwavutia watu kwenye dini ya Mwenyezi Mungu. Kwa kawaida, mtu hawezi kukaa mtulivu wakati anakabiliwa na hasira ya wengine na hasira mbaya. Hata hivyo, Nabii Nuh (AS) alikuwa na mtazamo wa kibaba kwa watu wake ambao walimdhihaki na kumsumbua.
Kwa mujibu wa riwaya, Nabii Nuh (AS) aliishi miaka 950. Kwa hiyo watu wake walimdhihaki na kumsumbua kwa karne tisa. Katika kujibu tabia hizo, alisema: “Akasema: Enyi watu wangu! Mimi simo katika upotofu, lakini mimi ni Mtume nitokaye kwa Mola Mlezi wa viumbe vyote. Nakufikishieni Ujumbe wa Mola Mlezi wangu, na ninakunasihini; na ninayajua kwa Mwenyezi Mungu msiyo yajua nyinyi.” (Aya ya 61-62 ya Surah Al-A’raf)
Licha ya matusi na manyanyaso aliyokumbana nayo, Nabii Nuh (AS) alizungumza na watu kwa wema na kuwaonea huruma, akitaka kulinda maslahi ya watu si yake.