IQNA

Qur'ani Tukufu Inasemaje / 51

Kushiriki katika Mashindano ya Kiroho

18:44 - May 17, 2023
Habari ID: 3477009
TEHRAN (IQNA) – Iwapo mtu atatuhimiza kuharakisha, tutamuuliza tuharakishe katika uwanja gani. Lakini wakati mwingine swali hili hili linaweza kutupeleka kwenye upuuzaji na kutufanya tuharakishe katika jambo ambalo si zuri kwetu.

Ulimwengu tunaoishi ni ule uliojaa harakati na shughuli za haraka na wakati mwingine tunaweza kujiuliza msukumo huu wote unahusu nini.

Ikiwa hatutajibu swali hili na badala yake kuendelea na uzembe au mghafala wetu, matendo na tabia zetu huelekea kwenye kutokuwa na maana na huwa  upuuzi.

Kuna aya katika Qur'ani Tukufu inatuambia tuharakishe. Inalinganisha juhudi za watenda mema na mashindano ya kiroho ambayo lengo lake kuu ni kupata msamaha wa Mwenyezi Mungu na baraka ya milele ya pepo.

Ni Aya ya 133 ya Surah Al Imran: “Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi, na Pepo ambayo upana wake ni mbingu na ardhi, iliyo wekwa tayari kwa wachamngu.”

Kwa kuwa haiwezekani kufikia cheo cha kiroho bila ya kupata msamaha wa Mwenyezi Mungu na kujitakasa na dhambi, lengo la mashindano haya ni kupokea kwanza Maghfira (msamaha wa kimungu) na pili kufikia pepo, ambayo ni kubwa kama mbingu na ardhi.

Kwa mujibu wa Tafsiri ya Qur'ani Tukufu ya Noor ya Hujjatul Islam Muhsin Qaraati, baadhi ya wanazuoni wanaamini kwamba pepo na moto tayari zipo na moja ya sababu zao za imani hii ni katika katika Qur'ani isemayo “iliyo wekwa tayari kwa wachamngu” katika aya hii.

Nukta nyingine katika aya hii ni kwamba kwa “Na yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi”, maana yake ni kuharakisha kutenda mema yenye kuleta msamaha wa Mwenyezi Mungu.

Katika tafsiri ya aya hii, Imam Ali (AS) alisema pitaneni katika kutekeleza majukumu yenu ambaye Mwenyezi Mungu amewaamurisha kuyafanya.

Ujumbe wa Aya ya 133 ya Surah Al Imran

  1. Kuharakisha katika mambo mema huongeza thamani yao: "Fanya haraka au yakimbilieni..."
  2. Kuharakisha kutubu na kutafuta msamaha wa Mungu ni muhimu. "Fanya haraka kupata msamaha kutoka kwa Mola wako Mlezi au yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi."
  3. Msamaha ni miongoni mwa utukufu wa Mwenyezi Mungu. “… msamaha kutoka kwa Mola wako Mlezi.”
  4. Mtu anapaswa kupokea msamaha kabla ya kwenda peponi. “Fanyeni haraka kupata maghfira kutoka kwa Mola wenu Mlezi na mpate kustahiki Pepo.
  5. Ili mtu afikie pepo ya wachamungu ni lazima awe miongoni mwa wachamungu.
captcha