Kupambana na aina mbalimbali za magonjwa na matatizo ya kifedha ni miongoni mwa changamoto zinazowakabili watu wote maishani. Changamoto hizi zinaweza kuwa majaribu kwa watu kwa sababu Mwenyezi Mungu anataka kuwajaribu. Wakati mwingine hutokea kama matokeo ya kutokuwa na shukrani kwa baraka za awali ambazo mtu amepokea. Kama vile shukrani huleta baraka nyingi zaidi, ukosefu wa shukran pia husababisha kupoteza baraka.
Mwenyezi Mungu anasema katika Aya ya 28 ya Surah Al-Baqarah: " Vipi mnamkanusha Mwenyezi Mungu na hali mlikuwa wafu akakufufueni! Kisha atakufisheni, tena atakufufueni, kisha kwake mtarejeshwa?."
Aya hii inasisitiza kwamba mwanadamu ambaye ni kiumbe dhaifu hapaswi kukataa kuwepo kwa Muumba ambaye hahitaji mtu yeyote na chochote. Baadhi ya mafunzo ambayo mtu anaweza kujifunza kutokana na aya hii ni kama ifuatavyo:
Mwenyezi Mungu amewakadhibisha wale wanaoishi katika ukafiri na wakafa katika ukafiri: “Hakika walio kufuru na wakafa hali ni makafiri, hao iko juu yao laana ya Mwenyezi Mungu na ya Malaika na ya watu wote." (Aya ya 161 ya Surah Al-Baqarah)